Font Size
Mathayo 26:31-35
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 26:31-35
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Asema Wafuasi Wake Watamwacha
(Mk 14:27-31; Lk 22:31-34; Yh 13:36-38)
31 Yesu akawaambia wafuasi wake, “Usiku wa leo ninyi nyote mtapoteza imani yangu kwangu. Maandiko yanasema,
‘Nitamwua mchungaji,
na kondoo watatawanyika.’(A)
32 Lakini baada ya kuuawa, nitafufuka Kisha nitakwenda Galilaya. Nitakuwa huko kabla ninyi hamjaenda huko.”
33 Petro akajibu, “Wafuasi wengine wote wanaweza kupoteza imani juu yako. Lakini imani yangu haitatetereka.”
34 Yesu akajibu, “Ukweli ni huu, usiku wa leo utasema haunifahamu. Utanikana mara tatu kabla jogoo hajawika.”
35 Lakini Petro akajibu, “Sitasema kwamba sikufahamu! Mimi hata nitakufa pamoja nawe!” Na wafuasi wengine wote wakasema kitu hicho hicho.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International